MTOTO HUANZA KUCHEZA LINI KATIKA TUMBO LA MJAMZITO.

MTOTO HUANZA KUCHEZA LINI KATIKA TUMBO LA MJAMZITO.

MTOTO HUANZA KUCHEZA LINI KATIKA TUMBO LA MJAMZITO.

Kwa kawaida akina Mama wajawazito huwezi kuhisi kucheza kwa mtoto tumboni katika umri tofauti tofauti kulingana Mama Mjamzito husika.

1. Mama Mjamzito ambaye hakuwahi kujifungua kwa maana kwamba Mimba yake ni Mimba ya kwanza,huwezi kuanza kuhisi mtoto kucheza tumboni kuanzia miezi 4½ hadi miezi 5.

2. Mama Mjamzito ambaye amewahi kujifungua au kubeba mimba Mara mbili au Mara tatu huweza kuhisi mapema zaidi kucheza kwa mtoto tumboni ambapo huhisi mtoto kucheza kuanzia miezi 4 au miezi 4½ ukilinganisha na wale ambao ni Mara ya kwanza kuwa na Mimba.

👉Ni vema kujua kwamba unapofikia umri huo wa mimba kuanzia miezi 4 kwenda juu uweze kuhisi mtoto akicheza tumboni na kama hata cheza baada ya umri huu utatakiwa kuwahi hospitali kupata vipimo zaidi.

❤️Kuanzia wiki ya 28 au miezi 7 ni muhimu mama kuhesabu kucheza kwa mtoto kila siku, endapo Mama Mjamzito huyu anaumwa magonjwa kama Kisukari,Magonjwa ya Moyo au shida nyingine ambazo zinaweza kupelekea hatari kwa Mama Mjamzito au Mtoto wake aliyeko tumboni.

Vile usikose kufuatilia video hii hapa chini

Umri wa Mimba ambapo Mtoto huanza kucheza Tumboni mwa Mjamzito.

Response to "MTOTO HUANZA KUCHEZA LINI KATIKA TUMBO LA MJAMZITO."

  • Je inawezekana ultrasound ikatoa majibu tofauti kuhusu umri wa mtoto kinyume na matarajio ya mama ? Kama kweli ni kwanini?

  • Mimi ni mjamzito nina mimba ya wiki 14 na siku 3 nilikua natumia style ya kulala chali kwenye tendo la ndoa je naweza nikawa nimemdhuru mtoto?

  • Nina ujauzito wa wiki 15 n siku kadhaa,nimekuwa na changamoto ya miscarriage ,mwenz wa 5 nlipata hiyo shida,nikabeba mimba tena mwez wa 9 .natoka nimebeba mimba nimekuwa nikitumia duphstone 2×2 kwa siku mpk.sasa n vidonge vy maumivu ya tumbo hyscine 2×3.kwa kila siku.kwa kuelekezwa n doct.je na maumivu y tumbo hayakomii n niko bedrest.swali langu nikutaka kujua hivi vidonge havitaleta madhara kwa mtoto?
    Asante.

  • Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *